Ugani na ushauri
Tunatoa huduma za ugani na ushauri wa kitaalamu kuhusu ufugaji wa samaki na viumbe maji kiujumla.
Fomula na uchakataji wa chakula
Mifugo na samaki wanahitaji chakula bora chenye kila kirutubisho kwa viwango sahihi ili mifugo yako au samaki wako wakue vizuri na upate faida yake. Tunatengeneza fomula za chakula cha mifugo na samaki kwa kutumia kompyuta kwa usahihi wa hali ya juu.
TEHAMA katika biashara na kilimo
Tunatengeneza programs za kompyuta kama website, mobile apps na mifumo mingine ya kurahisisha usimamizi wa biashara, miradi, na mashamba. Gharama zetu ni nafuu sana.
Tafiti na uchambuzi wa data
Tunafanya tafiti na kuchambua data (research and data analysis). Aidha tunasaidia wanafunzi kufanya tafiti na uchambuzi wa data kwa weledi wa hali ya juu.
Pia tunafundisha uelewa wa namna ya kutafuta, kupata na kutumia taarifa sahihi za kitafiti na za kitaalamu katika tafiti
Tunaandika maandiko ya tafiti na kufanya mapition na marekebisho ya kazi za tafiti
Mafunzo
Tunatoa mafunzo ya kompyuta (TEHAMA), ufugaji samaki, kilimo biashara, ujasiriamali, na Masoko.
Vifaranga na mbegu za samaki
Tunauza na kusambaza vifaranga vya samaki bora kabisha. Kifaranga kimoja kinapatikana kwa Tshs 200 tu
Miche ya miti na matunda
Miche ya miti na matunda inapatikana kwa Tshs 2500/= tu kwa mche mmoja.
Tunayo miche ya embe, papai, parachichi, limao, chungwa, pasheni n.k.
Tuyatunze mazingira kwa kupanda miti na matunda